Ndugu zangu tunapokaribia kumaliza mwaka huu wa 2018, hakika mioyo yetu imejaa shukrani kwa Mungu. Tunaweza kusema kwa ujasiri kabisa kuwa, “mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nasi”. Hatukubarikiwa tu kwa vitu vya kimwili bali pia vya kiroho, tumekua katika maisha yetu ya kiroho. Isitoshe, ulinzi wa Mungu umekuwa juu yetu. Tuseme nini basi, bali kushukuru.
Sasa tunapojongea kuingia mwaka mpya, mwaka uliokubalika mbele za Bwana, mwaka 2019, ninawiwa kushirikiana nanyi maneno machache tu kama kumbukumbu.